WhatsApp Group Join Now

Nafasi za Kazi za Mkataba Walimu wa Secondary 2025 Tunduru Dc

 

Nafasi za Kazi za Mkataba Walimu wa Secondary 2025 Tunduru Dc

Nafasi za Kazi za Mkataba Walimu wa Secondary 2025 Tunduru Dc

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri a Wilaya ya Tunduru anapenda kuwatangazia watanzania wote wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi za kazi za Mkataba a Mwalimu Ill , K w a Masomo ya Biashara(Nafasi 31),Kiingereza(Nafasi 02) na Historia( Nafasi 02).Hivyo anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa za kujaza nafasi hizo;-

Masharti ya Jumla kwa Waombaji wa Kazi

Waombaji wote wa nafasi za kazi wanatakiwa kuzingatia masharti yafuatayo kabla ya kuwasilisha maombi yao:


1. Uraia na Umri

  • Mwombaji lazima awe Raia wa Tanzania.
  • Awe na umri kuanzia miaka 18 hadi 45.

2. Waombaji Wenye Ulemavu

  • Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi.
  • Wanaombwa kuainisha aina ya ulemavu wao kwenye mfumo wa kuombea ajira kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

3. Wasifu wa Mwombaji (Detailed C.V)

Kila mwombaji anatakiwa kuambatanisha:

  • Maelezo binafsi ya kina (Curriculum Vitae - C.V).
  • Anuani halisi inayotumika.

  • Namba za simu zinazopatikana muda wote.
  • Anuani ya barua pepe (Email Address).
  • Majina ya wadhamini watatu (Referees) wa kuaminika.

4. Vyeti vya Elimu na Taaluma

Maombi yote lazima yaambatane na nakala zilizothibitishwa kisheria za vyeti vya kielimu na kitaaluma kulingana na kiwango cha elimu:

  • Cheti cha Kidato cha Nne (Form Four Certificate).
  • Cheti cha Kidato cha Sita (Form Six Certificate).
  • Vyeti vya Mafunzo ya Juu kama: Postgraduate, Degree, Advanced Diploma, Diploma au Certificate.
  • Computer Certificate.
  • Vyeti vya Kitaaluma (Professional Certificates) kutoka bodi husika.

5. Nyaraka Zinazokatazwa

Testimonials, Provisional Results, Statement of Results, na result slips za kidato cha IV na VI hazitakubaliwa.

Waombaji watakaowasilisha nyaraka hizo hawataruhusiwa kuendelea na usaili.


6. Waombaji Waliosoma Nje ya Tanzania

Vyeti lazima vihakikiwe na kuthibitishwa na mamlaka husika:

  • TCU – Tanzania Commission for Universities.
  • NECTA – National Examinations Council of Tanzania.
  • NACTVET – National Council for Technical and Vocational Education and Training.

7. Waombaji Waliofanya Kazi Serikalini

Waombaji waliostaafu kutoka Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.

Waombaji wanaoshikilia nafasi za kuingilia ndani ya Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba. Wanapaswa kuzingatia maelekezo ya Waraka Na. CAC.45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.


8. Taarifa za Kughushi

Waombaji watakaowasilisha nyaraka au taarifa za kughushi watakabiliwa na hatua kali za kisheria.


9. Tofauti za Majina kwenye Nyaraka

Waombaji ambao majina yao yanatofautiana kwenye vyeti na nyaraka lazima kuwasilisha Hati ya Kiapo (Deed Poll) kuthibitisha uhalali wa majina yao.

10. Mwisho wa Kutuma Maombi

Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 10 Septemba 2025.

Maombi yatakayowasilishwa baada ya tarehe hii hayatazingatiwa.


11. Utaratibu wa Kuwasilisha Maombi

Barua zote za maombi zitumwe kwa njia ya posta pekee kupitia anuani ifuatayo:

Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
48 Barabara ya Nalasi,
S. L. P. 275,
57682 – Tunduru.



Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Below Post Ad